BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Saturday, February 4, 2017

MWENYEKITI WA BODI YA WEZESHA TRUST FUND MZEE ODILO TWEVE ALIPOFANYA KIKAO CHA MIEZI MITATU NA WAFANYAKAZI WA WEZESHA TRUST FUND - OFISINI SABASABA MOROGORO

Wezesha Trust Fund ina kawaida ya kufanya vikao mara kwa mara na Mwenyekiti na wakuu wa Bodi yake ili kujadiliana kuhusu maendeleo na mustakabali wa Asasi hii.  Mwezi wa Saba, 2016 Mwenyekiti wa Bodi ya Wezesha Mzee Odilo Tweve alifanya kikao kujadili jinsi ya kufikia malengo yaliyowekwa na kukumbushana wajibu wa kila mfanyakazi wa Wezesha.

Mungu ni mwema kikao kilienda vizuri sana na majukumu yalifanyika kwa ufasaha sana, na maandalizi ya kutimiza miaka minne ya Wezesha yalipangwa na kuhakikishwa kuwa yatatimia katika mustakabali uliowekwa.

Pichani hapa chini ni Mwenyekiti pamoja na wafanyakazi wakijadiliana kwa kina kuhusiana na Asasi hii.

 Mwenyekiti Mzee Odilo Tweve akiongea kwa msisitizo mambo kuhusu miaka minne ya Wezesha Trust Fund nini kifanyike na kifanyike kwa namna ipi, wafanyakazi wakimsikiliza kwa weledi na utulivu mkubwa.

Mzee Boniface Mbogo nae ni mjumbe wa Bodi ya Wezesha Trust Fund akisikiliza kwa makini na akitoa hoja zenye mashiko makubwa kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa.  Abuu Mkingie mratibu wa mambo ya nje akitoa hoja zake za kuhakikisha atazungukia kila mahali kuweka sawa mambo yaliyopangwa kwa uweledi.
 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7