BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Wednesday, January 18, 2017

JE, UTAWEZAJE KUSHINDA HALI NGUMU YA MAISHA NA AJIRA




MBINU 6 ZITAKUSAIDIA SANA
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na hali ya kukua kwa uchumi mambo mengi yamebadilika sana, Hivyo basi ni muhimu tujifunze njia za kujiimarisha ili tuweze kupita salama katika hali hii, usipoteze muda kulalamika amka anza kuangalia mbinu hizi ili uboreshe maisha yako.  Nenda na dira usiwe mchelewaji wah sana uone faida ya kuwa wa kwanza katika kutatua matatizo na kupata fursa zilizopo karibu uone mbinu ambazo zitakusaidia kuinuka kiuchumi kwa haraka.

1. Uhuru wa fikra:  Kama kuna nyakati ambapo unahitaji uwezo wa kuiona dunia kama ilivyo na sio kama unavyotaka iwe, basi ni sasa. Ni muhimu kuboresha ufahamu wako wa mambo mengi ya kimsingi ya kimaisha kama vile mapenzi, biashara, tabia, teknolojia ,, na zaidi sana  maswala ya kiroho.
Uhuru wa kifikra utakuwezesha uweze kujitawala vema, kwani kimsingi wewe ndiye mtu wa kwanza kabisa unayeweza kuleta mabadiliko makubwa na maendeleo kwa maisha yako, kwakuwa unayo nguvu ya utashi,  kufanya maamuzi au kuacha watu waamue mambo kwa ajili yako.

2. Kuboresha mtandao:  Kwakuwa unahitaji kutambua fursa nyingi kwa kadri inavyowezekana na kwa kuwa wewe ni mzalishaji, unahitaji sana kujenga mtandao mkubwa na mtandao wenye manufaa ili kuweza kutambua fursa mbalimbali kupitia mtandao wako, na pia kuweza kuuza bidhaa zako kupitia mtandao huo.  

3. Kuwa mzalishaji: Katika machafuko haya, bidhaa na huduma mbalimbali zitakuwa adimu, na kwa wazalishaji wachache watakaoweza kuzalisha kwa ufanisi wataweza kujikuta wakiendesha maisha vizuri.  Hivyo pamoja na kuwa mtumiaji wa fedha zako kwa mambo ya burudani, unahitaji kuhifadhi fedha zako kwa namna ambayo fedha zako hazitopoteza thamani zake, na wakati huo huo, ukifanya utafiti wa aina ya bidhaa au huduma ambazo utakuwa ukizalisha, ili nawe unufaike na mazingira tuliyonayo.  Kuendelea kuwa muingizaji wa kipato (kwa njia ya ajira pekee) na kuwa mtumiaji zaidi ya mwekaji akiba, si jambo la busara, hasa katika hali ngumu ya kiuchumi na kijamii tuliyonayo.

4. Kuwa mwepesi wa kubadilika: Mambo mengi yanabadilika kwa haraka sana, ufahamu uliokuwa nao jana , mbinu ulizotumia siku za nyuma  hata kama zilifanikiwa, inawezekana kabisa zisifanikiwe kwa sasa, na kwa kadri mambo yanavyozidi kubadilika. Ushindi wa kipekee unakuja pale unapoweza kuwa mwepesi wa kubadilika, kwa kubuni njia mpya na bora za kukabiliana na mazingira unayokumbana nayo.

 

5. Kaa tayari kwa kusafiri:  Fursa zinaweza kutokea popote pale, hivyo kuwa tayari kusafiri nje ya mkoa uliopo sasa, na zaidi sana nje ya nchi. Hakikisha una passport halali na isiyoisha muda wake, na tambua taratibu za kusafiri nje ya nchi, kama vile mambo ya visa,  na gharama za maisha kwa nchi tofauti.  

6. Mipango ya muda mrefu: Tambua kuwa hali hii ngumu ya maisha ni swala ambalo litaendelea kwa muda mrefu, hivyo ni muhimu kujipanga wewe na familia yako. Kama una watoto au una mpango wa kuwa na watoto, basi ni wakati wa kufikiria pia namna ya kuja kuwawezesha watoto wako wawe na ujuzi wa uhakika, na kuwa wawe wazalishaji.  Hakikisha unajitengenezea ujuzi na uzoefu uliokomaa katika jambo fulani au mambo kadhaa tofauti, ili uweze kuja kuuza ujuzi na uzoefu wako huo katika soko gumu la huduma tunalokumbana nalo kwa nyakati za leo na zijazo.

Lusako Mwakiluma
Muhamasishaji na Muinuaji
January, 2017


Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7