BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Tuesday, December 27, 2016

WEZESHA TRUST FUND - MOROGORO YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA

WEZESHA TRUST FUND WALIPOTEMBELEA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA BIGWA - MGOLOLE
TAREHE 26/12/2016. 
WALITOA MISAADA  MBALIMBALI KUSHEREHEKEA SIKU YA KUFUNGUA ZAWADI 
 PAMOJA NA WATOTO HAO   
WALITOA MISAADA YA SAMAKI, NYAMA, MATUNDA, SABUNI, SUKARI NA VINYWAJI MBALIMBALI  


Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund - Morogoro wakisaini kitabu cha Wageni Bigwa Mgolole - Kituo cha kulelea watoto yatima kutoka kushoto Mkurugenzi Bi Lusako Mwakiluma, Daktari Dr Elias Yuda Mtungilwa, Msaidizi wa Utawala na Mwalimu wa Tehama Maines Richard, Afisa Mafunzo Mohamed Nyongo.

Wezesha Trust Fund wakifurahi pamoja na  Sista mlezi pamojawatoto yatima mara baada ya kukabidhi misaada, watoto walifurahi sana kupokea zawadi zao.

Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund wakiwabembeleza watoto yatima ambao ni wachanga wanaolelewa katika kituo hicho, 

 Wezesha Trust Fund kwa pamoja inaiomba jamii kuwa na tabia ya kuangalia watoto kama hawa katika vituo vilivyo karibu na mbali kwani ni faraja kubwa kuhakikisha yatima wanapata furaha kama watoto wengine.  Yatima ni watoto wetu tusiwatenge wala kuwabagua.
Wezesha Trust Fund wakiwa pamoja na watoto yatima wa darasa la kwanza na pili - kituoni hapo wakiongozwa na Derick na David(mapacha) ambao tangu wakiwa na siku tatu baada ya kuzaliwa na kufiwa na mama yao Wezesha inawatembelea na kila wanapowaona wafanyakazi wa Wezesha wanafurahi sana.
Mungu wabariki walezi wa watoto hawa yaani Masista wote wanaohusika na pia wabariki watoto yatima wote wakue katika maadili mema na kumtegemea Mungu.

Sunday, December 25, 2016

USIMKOPESHE RAFIKI AU NDUGU YAKO

Kwa nini leo nimefikiria haya?  Naomba nikwambie pesa ni jawabu la mambo yote namadhambi yote yameanzia kwenye pesa.   Unaweza kuwa na rafiki au ndugu mliyeshibana sana lakini pesa ikaja kuwatenganisha kwa urahisi mno na mkachukiana milele.  Pesa inatengeza marafiki na pia inaleta uadui ndani yake.  Basi ili uishi kwa amani kila kitu unatakiwa ukifanye kwa kiasi. 

Kila wakati fanya msaada wa kipesa kama zawadi usifanye kama mkopo.  Kama haujampa mtu  msaada wa kipesa urafiki wenu unaenda kuisha taratibu. Kama uko kwenye eneo la kuweza kumsaidia mtu basi msaidie usimkopeshe mpe tu.  Na kama unajua hauwezi kumpa usimkopeshe itaenda kukuumiza wewe mwenyewe
(Ron Henley).

Sababu ya kutompatia mkopo rafiki au ndugu wa karibu ni kwasababu ya kuondoa usumbufu usio wa lazima wa kudaiana pasipo mashiko. Uhusiano wenu unaenda kuvunjika kama sio kuharibika kabisa.  Sababu ya watu inayowapelekea kupata matatizo ya kipesa ni kutojua jinsi ya kufanya kazi na pesa au jinsi ya kutumia fedha.  Ukiwakopesha wala hawajui wanaenda kufanyia nini kwani hawajajiandaa cha kwenda kufanyia hizo pesa. 
Kabla ya kufahamu hivyo watachukua pesa kwako tena wataanza kutoa udhuru wa kushindwa kukurudishia.  Kinachofuata hapo ni kukukimbia kila wanapokuona.  Kuacha kupokea simu yako na mwisho kutofungua mlango mara unapopiga hodi majumbani kwao.

Naomba kwa ushauri kama unataka kumsaidia ndugu yako au rafiki mpatie pesa kama msaada na sio mkopo ili uishi kwa amani kwani utakapomkopesha hiyo pesa usiihesabu katika akiba yako kwani imeondoka na hauwezi fahamu itarudi lini. 
Hii ni kwa faida yako ya watu wengine.

Karibu tusaidiane pale tuliposhindwa na tunapoweza tuelekezane.

Kwani maarifa ni mali kuliko pesa.

Lusako Mwakiluma
Mhamasishaji na Muinuaji kwa waliokata tamaa na kuugua

27 Desemba, 2016

JE, KUWA TAJIRI KUTAKULETEA FURAHA

Kwa nini unataka kuwa na pesa nyingi, je pesa nyingi zitakupatia amani au furaha? 
Kuwa na pesa nyingi itakupatia amani.   Kama utakuwa na pesa nyingi  utalipa madeni yako yote, utakwenda popote unapotaka kwenda na utafanya chochote unachotaka kufanya.

Ninachotaka kukufahamisha  hapa ni kwamba kuwa na pesa nyingi itakusaidia  kuponya vitu vyote?  Usije ukaanguka mwenyewe kwenye eneo la kufikiria. Kama unafikiria pesa itakupatia furaha, utakuwa unajidanganya mwenyewe.

Hauwezi kuwa na furaha utakapokuwa na pesa nyingi labda unaweza kuwa na furaha usipokuwa na pesa.  Kama ni mtu mwenye kumaanisha, kuwa tajiri kutakufanya uwe na uhuru wa kujiamulia mambo yako mwenyewe kwa kile ulichonacho kwa wakati ule.  Kama utakuwa mtu mwenye huzuni, kuwa tajiri utakuwa  umejipa uhuru wa kuitafuta furaha yako kwa wakati huo.

Kuwa tajiri ni kwamba tayari umeshaandaa kiasi cha pesa ambacho ulikitafuta.  Ufahamu wako utakuwa unajihakikishia kuwa mtu ambaye hapo mwanzo haukuwa hivyo na cha muhimu ni kuvunja sheria ya kujipangia matumizi yako ya pesa kabla ya kuishika mkononi.
Mfano:   30% kwa ajili ya matumizi ya kuishi
                30% kwa ajili ya matumizi ya kuweka akiba
                30% kwa ajili ya matumizi ya starehe na furaha ya  familia
                10% kwa ajili ya kuwapatia wasionacho
Asilimia mia moja (100%) ya kila pesa yako igawanye katika mafungu manne.

Kitu cha muhimu sana ni kufanya kazi kwa bidii yako mwenyewe kuliko kufanya kazi kwa ajili ya kutafuta utajiri.  Ni muhimu kufanya hivyo kwasababu kiasi cha utajiri  wa mtu alichonacho hakiwezi kuzidi  maendeleo yake binafsi.
Ngoja nikupe mfano:  Ni mara ngapi unasikia mtu ameshinda bahati nasibu na amepata kiasi kikubwa cha pesa?  Halafu baada ya muda mfupi unasikia zile pesa zote zimeisha kwa muda mfupi sana.

Kumbuka alikuwa anasema kabla ya kuzipata pesa hizo.  Kama nikishinda kiasi kikubwa cha pesa kwenye bahati nasibu nitafanya kitu kikubwa na nitakuwa tajiri mkubwa sana, kumbuka alisema wakati hajazishika hata wewe wakati hauko na pesa unasema nikizipata.  Je, umepanga chochote kabla ya hizo pesa kupatikana au utapanga ukishazipata? Utafiti unaonyesha kwamba bahati nasibu ni kitu kinachojulikana sana na watu wanaamini katika bahati nasibu kwa sababu mbili:
            1. Mpango wa pesa za haraka haraka
            2. Pia ni mchezo wa furaha

Ni mchezo unaochezwa kila siku leo unaweka pesa kidogo na kesho unapata kiasi kikubwa basi ni kitu endelevu na watu wanategemea kuna siku nitapata zaidi ya jana.  Hii inakuhakikishia kama utapata basi utamaliza shida zako zote. Na yale yaliyosimama yote yatafanikiwa kwa urahisi. Watu wengi wanaandaa kesho yao kwa kujinyima leo ili kesho yao iwe nzuri zaidi.

Hauwezi kuwa tajiri mpaka uvunje sheria kwa kujihakikishia kila pesa yako unayoipata unaivunja mara nne ili uweze kutimiza azma yako uliyojiwekea. Nitakuletea mpango mzima wa kuwa tajiri kwa haraka kwa kuvunja sheria.

Karibu sana tuchangie hoja, tutoe maoni na tujihakikishie kufika pale tunapopataka.

Lusako Mwakiluma
Mhamasishaji na Muinuaji kwa waliokata tama
Wezesha Trust Fund - Morogoro

26 Desemba, 2016


Sunday, December 11, 2016

FORTUNE TEAM WAKIFANYA USAFI SABASABA HOSPITAL - MOROGORO


Wezesha Trust Fund wakiwafundisha kazi za kujitolea Fortune Team kutoka shule ya sekondari Uwanja wa Taifa siku ya 1 Desemba, 2016 kuazimisha siku ya Ukimwi Duniani, Timu ya Fortune inafahamu jinsi ya kusema hapana na kujikinga na VVU/Ukimwi wakiamini Vijana bila ukimwi inawezekana.

Fortune Team wakiendelea na kufanya usafi kwa kujitolea kama walivyofundishwa na Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund - Morogoro
Fortune Team wakiendelea na usafi baada ya kuhitimisha mafunzo yao ya siku Moja ya kuepuka na kujikinga na Ukimwi mashuleni.

Mkurugenzi wa Wezesha akihakikisha kwamba usafi unafanyika kwa kiwango cha hali ya juu katika Hospitali ya Sabasaba ndani ya kata ya Uwanja wa Ndege.


 Mohamedi Nyongo afisa  Mafunzo akishirikiana na Fortune Team kufanya usafi kwani mtoto umleavyo ndivyo akuavyo na mifano ni lazima kwa wanafortune team.  Mungu ibariki Wezesha na Mungu ibariki Fortune Team.
 Mkurugenzi wa Wezesha Trust Fund akihojiwa na Vyombo vya habari kuhusiana na siku hiyo.  East Africa Radio na Television walikuwepo pia SUA Television walisimama kidete kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa sawa.
Afisa Tawala Bi Mainess Derick akiwa pamoja na Fortune Team kwa msisitizo wa siku ya Ukimwi Duniani wakiamini kuwa maombukizi mapya ya Ukimwi kutoongezeka na kuhakikisha yanapungua kama sio kumalizika.

Ilikuwa ni siku ya Ukimwi Duniani 1 Desemba, 2016

Fortune Team ni wanafunzi toka Shule ya Sekondari Uwanja wa Taifa waliojiunga na Wezesha Trust Fund kama mabalozi wa wanafunzi wengine katika kuhakikisha wanafuata maadili ambayo nao wamefundishwa na kuelimishwa na Wezesha Trust Fund - Morogoro ikiwa ni muendelezo wa kazi ya kuwaelimisha Vijana rika kuweza kufanikiwa katika malengo yao waliyojiwekea kwa kuepuka vishawishi toka kwa wanawake na wanaume, mimba na ndoa za utotoni, Semina ilifanyika tarehe 19/11/2016 katika Ukumbi wa Pastor Phil Training Centre.

Mambo matano waliyojifunza:

1. Elimu ya Kujitambua
2. Jinsi ya kuepuka mimba na ndoa za utotoni
3. Elimu ya Ukimwi na VVU na jinsi ya kuepuka
4. Jinsi ya kusoma na kufaulu kwa kiwango cha juu
5. Elimu ya kufanya kazi za kujitolea

Wezesha pia inawashukuru Viongozi wa Mkoa wa Morogoro kwa ushirikiano wa siku hii ya usafi kwani ilikuwa ni kuwafundisha vijana hawa kufanya kazi ya kujitolea katika jamii kwa hiari yao.  Tunashukuru Mkurugenzi wa Manispaa, Mganga Mkuu wa Mkoa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sabasaba kwa ushirikiano waliotupatia.  Tunasema asante sana.  Kauli mbiu ya siku ya tarehe 1 Desemba, 2016 saidia kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi. 

BOFYA HAPA KUONA TUKIO LA SIKU YA WEZESHA

NJIA TANO ZA KUONGEZA UJASIRI WAKO

1.   Chagua watu wenye ujasiri na wenye hari ya chanya ndani yake
Kaa na watu wenye ujasiri, ukikaa na watu wenye ujasiri nawe utakuwa jasiri kwani utajifunza kupitia wao kumbuka hata Biblia inasema enenda na wenye hakima nawe utakuwa na hekima mithali 13:20 lakini rafiki wa wapumbavu atahangamia.

2.     Fanya kila siku kitu kinachokufurahisha au kukifurahia. 
Ukifanya kitu ambacho haupendi kufanya hauwezi kutunza ujasiri wako, utakuwa unafanya huku haujiamini.  Fanya kile kitu roho yako inataka na utaona unakifanya katika hari kuu na kubwa sana.

3.     Zingatia malengo na mipango uliyojiwekea
Malengo ni muhimu sana katika maisha ya kila binadamu.  Kama hauna malengo basi amini kwamba ufahamu wako umekufa.  Malengo na mipango yako ndiyo inayokupelekea kufika mbali kimaisha.  Hauwezi kufanya mambo kiholelaholela.  Mipango ndiyo matumizi yako ya kila siku.  Mipango na malengo ni dira ya mafanikio yako.  Andika kwenye daftari au kitabu malengo yako kisha uyafanye kwa mpangilio unaoutaka kwa muda uliojiwekea.

4.     Usikate tamaa
Katika safari ya maisha hakuna kukata tamaa na mtu jasiri hakubali kushindwa kwa lolote.  Hivyo hata kama unaona kuna kushindwa usikate tama kabisa.  Songa mbele uweze kuiona siku nyingine na mwisho kufikia malengo uliyojiwekea.

5.     Tumia muda wako vizuri
Muda ni pesa, na wakati ni mali masaa 24 tuliyopewa na mwenyezi Mungu wote tunayo.  Iweje tajiri afanikiwe kwa masaa haya haya 24 na wewe ushindwe katika masaa haya 24 inabidi ujiangalie tena na tena.  Pia usiogope kujaribu kwa kuhofia kushindwa kwa muda uliopo, unaweza ukashindwa kumbe ndiyo ushindi wako unapoanzia. 

Karibu sana tuendelee kuinuana na kutiana nguvu.

Lusako Mwakiluma
            (Motivational & Inspirational speaker)
                 


BOFYA KUPATA HABARI YA KUMJALI MTEJA

Tuesday, October 4, 2016

KILA NYUMA YA MWANAMKE JASIRI YUKO YEYE MWENYEWE



Kama watu wana wasiwasi kwa ukubwa wa mafanikio uliyonayo,  wewe endelea kufanikiwa zaidi  hautawasikia tena wakisema kuhusu wewe.

Maisha ya mwanamke shujaa/Jasiri yana ushuhuda mkubwa sana, ukimkuta mwanamke amefanikiwa basi ujue kuna kitu amepitia pamoja na machozi yake atajifuta kisha atasema nina nguvu, sio kila unamuona kafanikiwa unataka uwe kama yeye, kama inawezekana muulize safari yake atakuambia ni safari ndefu yenye milima na mabonde lakini mwisho wake atakwambia niko peke yangu pamoja na yote haya. “nyuma ya mwanamke jasiri yuko peke yake”. 

Huwezi kuwa jasiri kama mwanamke halafu ukawa na mtu nyuma yako ni wewe tu, kwani wanawake wengi hawataki mafanikio kama yako ila wanataka habari zako na kukutangaza kwa mabaya yako.  Naomba mwambie Mungu muweza wa yote kwamba ili nalo litapita.  Kwani hakuna jambo lisilo na mwisho katika maisha ya mwanadamu yeyote awe mzungu, burushi au budha, Muhindi hata Mbantu.  Endelea kumuomba Mungu siku zote,  muomba Mungu hachoki.

Mpendwa wangu, mwanamke mwenzangu naomba nikuhakikishie simama katika nafasi yako, fanya kazi kwa bidii jiamini peke yako, watu ni wengi lakini binadamu ni wachache.  Acha tufanye kazi kwa faida yetu wenyewe na familia zetu.  Kwani mtafutaji hachoki na hakichoka amepata, hata Bakhresa ana pesa lakini bado anatafuta usiku na mchana.  Mtangulize Mungu katika kila jambo lako.  Naye atakupa unachokitaka kwa wakati wake.


Lusako Mwakiluma
Motivational & Inspirational Speaker
Wezesha Trust Fund - Tanzania


Friday, September 9, 2016

MECHI KATI YA POLISI MORO NA MAWENZI MARKET SIKU YA WEZESHA DAY AGOSTI-2016

Bonanza lililofanyika siku ya “WEZESHA DAY” ni Mechi kati ya Mawenzi Market na Polisi Moro lilidhaminiwa na Wezesha Trust Fund ili kuchangia kufanya utafiti na kukuza vipaji kwa vijana wetu kwenye Muziki wa kuimba na kucheza.  Mgeni Rasmi wa Shughuli nzima alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi – Wezesha Trust Fund Mheshimiwa Odilo Tweve.

Mheshimiwa Odilo Tweve alisema; nanukuu ndugu wanajamii nawaambia michezo ni afya, michezo ajira, michezo pesa na michezo ushirikiano na mshikamano katika jamii, tunakutana, tunabadilishana mawazo pia tunafurahi pamoja.  Hivyo basi tuendeleze vipaji vya vijana wetu ili tuweze kuwanusuru vijana waishio katika mazingira hatarishi, kwani watoto wa mazingira hatarishi tunawapenda na ni watoto wetu, tuwakimbilie, tuwahoji na tuwasaidie ili kujenga Taifa la Tanzania.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wezesha Mheshimiwa Odilo Tweve, akitambulishwa wachezaji wa Polisi Moro na Mawenzi Market kabla ya Mechi kuanza.
Mwenyekiti wa Bodi Mheshimiwa Odilo Tweve akiwaasa  wachezaji kabla ya Mechi kuanza kati ya Polisi Moro na Mawenzi Market  siku ya Wezesha Day


Wachezaji wakisikiliza kwa  makini ushauri nasaha kutoka kwa Viongozi wa Wezesha Trust Fund - Morogoro kwani michezo ni afya, michezo ajira na michezo ni ushirikiano na mshikamano.

  SHUKRANI KWA JAMII

Tunapenda pia kuwashukuru wote waliotuunga mkono kwa hali na mali ili kufanikisha shughuli nzima kwani tumemuona Mungu kwa namna ya tofauti na na tunaihakikishia jamii kwamba lazima watoto waishio mazingira hatarishi wapate muafaka wa matatizo yao kama sio kwisha kabisa. Kwani tulichopata si haba kuweza kufanikisha  malengo ya watoto na vijana hawa.

KAULI MBIU YA WEZESHA DAY:

“Watoto waishio mazingira hatarishi tunawapenda”


Lusako Mwakiluma
Mkurugenzi
Wezesha Trust Fund

Kwa niaba ya Bodi ya Wezesha na Wafanyakazi wote.

Umoja ni Nguvu, Utengano ni dhaifu

“HAPA KAZI TU”

WEZESHA TRUST FUND KUTIMIZA MIAKA MINNE KWA USAFI NA BONANZA - MOROGORO


Wezesha Trust Fund imetimiza miaka minne tangu kuanzishwa Agosti, 2016  kwa kuwa karibu na Jamii inayoizunguka kama vile Hospitali ya Sabasaba iliyoko katika kata ya Mafiga na Uwanja wa Taifa, nia na madhumuni ni kuonyesha mfano kwa jamii  kwamba tunatakiwa tufanye usafi katika maeneo yetu bila shuruti tukiamini usafi unaanzia nyumbani.  

Wezesha ofisi zake ziko Kata ya Uwanja wa Taifa, pia Wezesha ni Asasi ya kijamii ambayo inafanya kazi pamoja na wanajamii  na kupitia kazi hizo kunaifanya Wezesha kujua matatizo ya jamii inayoizunguka na kuweza kuyatatua yale yaliyo ndani ya uwezo na yale yaliyo nje kuyapeleka kwa Serikali - Kiwilaya na Kimkoa ili kuweza kuyapatia ufumbuzi wa kina.

Pia iliandaa Bonanza kubwa la Mpira wa Miguu na kuinua vipaji kwa vijana katika muziki, kuimba na kucheza ili kuweza kuwapeleka mbele zaidi.  Mechi kati ya Mawenzi Market na Polisi Moro ilichezwa na makusanyo ya kiingilio kilichopatikana yalienda kusaidia  kufanya utafiti kwa waishio katika mazingira magumu  wanaofanya shughuli zao Mawenzi Sokoni na nyingine zitawaandalia stadi za kazi baadhi ya watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane(18) na wale wakurudi shuleni chini ya umri wa miaka (18) watarudishwa kwa mujibu wa sheria.


Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund wakifanya usafi katika Hospitali ya Saba-Saba Mkoani Morogoro katika kuadhimisha siku ya WEZESHA DAY - AGOSTI, 2016.  Tukianzia na kushoto ni Mkurugenzi Bi Lusako Mwakiluma, Abubakari Mkingiye, Mohamedi Nyongo, John Ndumbalo, Wellingtone Maselle na Salum Tindwa. 

Tunakwenda sambamba na  Kauli mbiu ya Rais wetu Mheshimiwa Dr John Pombe Magufuli.  
Hapa Kazi tu!!!


Lusako Mwakiluma
Mkurugenzi
Wezesha Trust Fund

Kauli Mbiu - "Wakiwezeshwa wanaweza"

Sunday, March 20, 2016

FIKIRIA KAMA MBUNIFU ILI UWE MTU MWENYE UMAKINI WAKATI WOTE

Wakati unafikiria mawazo yako ya ndani ni kwamba uko tayari kuzalisha kitu kizuri ulichobuni kama mbunifu;  Wakati wote unatakiwa kuwa hivyo ili uweze kuleta kitu cha tofauti katika jamii. Waangalie wabunifu wakubwa walioweza kutumia umakini na kuweza kubuni baadhi ya vitu ambavyo leo tunavitumia;-

Thomas Edison alifikiria akapata wazo kubadilisha ulimwengu wa Technolojia
Albert Eistein alifikiria akapata wazo la kubadilisha ulimwengu wa fizikia
Charles Darwin alifikiria akapata wazo la kubadilisha ulimwengu wa biolojia

Sio wote kwa upande wetu wanafanikiwa kwa kiasi cha kupata wazo zuri, tunaangalia kwa kufikiria ubunifu, mawazo mazuri na kupata suluhisho la jambo.

Kufika hapo unatakiwa uende kufikiria kila siku na uangalie ubunifu wako wa ndani kwa kutengeneza mawazo mengi na kuchukua kama tahadhari kama inawezekana.

Hapa angalia jinsi ya kutengeneza mawazo kama mbunifu:
Fikiria sana
Tengeneza mawazo mengi, mbadala na mwisho wake kama inawezekana usiwe na wasiwasi kuhusu  ubora wa wazo lako, ila ni mawazo mangapi unaweza kuwa nayo.  Kuna muda wa kuangalia tena baadaye na hata kama umemaliza kuyaangalia mawazo yote.  Kitu unachokitaka hapo ni kupata wazo moja tu kubwa.
Usijihukumu
Hata kama ukoje au upendi mawazo yako yaache yaje.  Kuangalia somo la nyuma kwa macho mapya, kama ulipitia kwenye hali hali ngumu jaribu kutazama kwa mtazamo mwingine mpaka upate wazo moja zuri. Hii itakusaidia kufikiria kitu katika ufahamu wako ambao huru, usijihukumu.
Tengeneza orodha
Andika chini au pengine tunza kwenye kumbukumbu kila wazo, hata kama unaona sio wazo zuri kwako.  Tena  wazo baya  unaliweka pamoja kwani ndani yako sio yote mawazo mazuri kama linakuja liweke tu unaweza ukalitumia mahala fulani na usijiweke katika sehemu ya kuchanganyikiwa kuhusu mawazo yako, subiri au  jiulize ni wazo langu mwenyewe? Baadaye unaweza ukaitumia hiyo orodha kupata faida kubwa.

 Changanua mawazo yako na uyaboreshe
Njoo na mtazamo wa wazo lako kwa kulipanga bila kufuatana au kutokuwa na umuhimu.  Angalia njia mbadala ya kufikiria kuhusu  somo hata kama  ni njia ya zamani lakini inafanya kazi.
Pika wazo lako na  na liiache liendelee mpaka lizalishe kitu
Panga muda  wa kupika  mawazo yako na yaruhusu  yaweze kuendelea kuzalisha mawazo mengine hii inachukua muda.  Fanyia kazi tatizo, tengeneza wazo, tena tembea  na fanya kitu kingine kabisa tofauti. Usifikirie kuhusu tatizo  wakati mwingine ila liache nyuma tatizo likiungua polepole. Unaweza ukashangaa ni wakati gani ndani kitu kinafanyika chenyewe, wakati wewe umeacha kiendelee chenyewe.

Wote tunataka kupata ubora mzuri na mawazo mazuri katika kila tunachokifanya.  Ili kuboresha njia nzuri ni kufikiria sana na jinsi tunavyojiongoza na jinsi tunavyoutunza muda wetu, hatua ya kwanza ni kuboresha  tunavyofikiria.  Je, unafahamu hivyo? Nakwambia utakuwa mtu mwenye umakini katika kila unachokifanya wakati mwingine popote ulipo.


Lusako Mwakiluma

Friday, March 11, 2016

MAISHA NI SAFARI YENYE MILIMA NA MABONDE

Wapendwa naamini kwa uwezo wa Mungu mmeshinda salama, leo napenda kutoa mada fupi na ya kutiana moyo wenyewe kwa wenyewe, kwa mtazamo wa macho ya nyama maisha ni magumu sana, lakini katika mtazamo wa kiroho maisha ni ya kawaida na hayataki mashindano, unashindana na nani? Na unaishi kwa ajili ya nani?  Fanya kile kitu ambacho kina manufaa kwako na familia yako ili kesho uje uburudike.  Kwani kuishi ni leo kesho ni matokeo unaweza ufike au usifike, jiwekee akiba kama vile unaishi milele halafu muofie Mungu kama vile unaondoka(kufa) leo.

Watu wengi wamechukua muda mrefu kutafuta furaha wameikosa, furaha inaanzia ndani mwako (happiness is inside job) usikae ukisubiri mtu kukupa furaha, utaipata furaha ya muda, jiangalie unataka nini na unaweza kufanya nini katika maisha yako?  Jitume sana, fanya kazi sana ili uweze kula matunda mema ya nchi.  Na kumbuka tunaufukuza upepo inabidi tuweze kumshukuru huyu anayetupa pumzi ya bure kwa neema na rehema zake, wengi wanalia, wengi wamekata tamaa, wengi wanataka kujiua na wengine wamesusa hata kuanza tena kwa kuanguka.  Mwenye haki wa Mungu huwa anaanguka mara saba kisha anainuka tena.  "With God there is second chance".

La hasha wakati ni huu tuamke na tutende yale tuliyoyandika kwenye vitabu vyetu kama ni malengo ya mwaka 2016 najua kuna wengine hawajaandika na hawana tabia ya kuandika malengo yao. Maandishi yanadumu milele, mazungumzo ni muda mfupi tumia muda wako kuandika malengo yako na uyafanyie kazi, "see it, believe on it, then you should act on it and you shall see the results as soon as possible"

Hii ni changamoto kwani kila siku angalia umefanya nini na ikifika jioni piga mahesabu ya masaa uliyotumia  kwa kufanya kitu hata kimoja cha maana "Do one good deed a day"

Wako muuinuaji na mtia watu moyo hata kwa yale yanayoonekana magumu, imani pasipo kuona itakupatia majibu ambayo ukufikiria.

Lusako Mwakiluma

Saturday, March 5, 2016

WANAWAKE NA FURSA-UJUMBE KWA WANAWAKE WA TANZANIA 8 MACHI, 2016

Tanzania ni mwanachama mwaminifu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki – Kutokana na milango kuwa wazi sasa Mheshimiwa Rais wetu Magufuli ametuhakikishia tunaweza kuvuka mipaka na kujitanua kupata fursa zaidi. Katika kuadhiminisha siku ya wanawake Duniani - Wanawake wa Tanzania tuinuke na tujihakikishie kushiriki kikamilifu katika ubunifu wa biashara endelevu ambazo zitakuwa na viwango vya kukidhi matakwa ya kijumuiya, tuache kutengeneza bidhaa za kuishi muda mfupi na zisizo na ubora. Fursa zinatutembelea tuwe wasomaji wa magazeti na vitabu hata mitandao ya kijamii ili tuweze kujipatia mbinu za kutengeneza na kuuza  bidhaa za aina mbalimbali ambazo ni za kwetu wenyewe na sio kuchat na kudadisi tu kupitia mitandao muda wote, tuitumie hii mitandao kwa manufaa ya kutangaza biashara zetu wenyewe. “HAPA KAZI TU”.

Tumehakikishiwa kwamba bidhaa za ndani sasa zimepewa kipaumbele, ebu tuamke na kukimbilia Taasisi za fedha kama vile CRDB, NMB, NBC, EXIM, BOA, POSTA, FINCA, BLACK na BLUE na Taasisi zingine za fedha kuweza kuchukua mikopo yenye tija kwa uzalishaji wa uhakika.  Wanawake tunaweza sana, tuache hofu na uoga wa kushindwa.  “Sikuzote  asiyekubali kushindwa sio mshindani”.

Maisha ili yawe mepesi wanawake  tunatakiwa tujitoe kwa hali na mali, kinamama tuwe mfano kwa kizazi kijacho kwa kujihakikishia tumejipanga kufika mbali katika biashara zetu ili kuinua uchumi wetu na familia zetu. Tukifanya biashara zetu sisi ndio tutakaoweza kuwaandalia watoto wetu maisha mema na yenye tija. Tunaweza kuchangia madawati, madaftari na vitabu vya kiada vya watoto na huduma nyingine nyingi katika jamii yetu. Kwani ukimwelimisha mwanamke umeielimisha jamii nzima na pia kila mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake kuna mwanamke.  Tunalilia usawa basi na tukimbilie fursa kwa usawa.

Tanzania wanawake ni wengi sana hasa wafanyakazi na wafanyabiashara, kwa wale waliofanikiwa tuwafundishe wengine mbinu za kuweza kujiinua kwa urahisi na kufikia malengo. Maarifa ukimgawia mwingine unafanikiwa zaidi tuondoe ile hari ya wivu na masengenyo wakati wote sisi kwa sisi.  Tuwe tayari kuwauliza wanawake waliofanikiwa njia gani wamepita au wanapitia ili tuweze kujifunza kupitia wao.  Wanawake tuwe wazuri katika kurejesha mikopo katika Taasisi za fedha kwani wanawake wengi wanakopa na kukimbilia Taasisi nyingine na kuacha madeni yasiyolipika. Mafanikio hayakimbiwi ila mafanikio yanakimbiliwa.

Naamini ujumbe huu utawafikia wanawake wa Tanzania nzima ili tuamke na kuchangamkia fursa zozote zinazojitokeza kwa kipindi hiki cha “HAPA KAZI TU” kwani asiyefanya kazi na asile.

Wanawake tunaweza.

Lusako Mwakiluma
MKURUGENZI WEZESHA TRUST FUND


Monday, February 29, 2016

MAISHA NI RAHISI SANA UKITULIA NA KUTAFAKARI

Napenda kutoa mada fupi na ya kutiana moyo wenyewe kwa wenyewe, kwa mtazamo wa macho ya nyama maisha ni magumu sana, lakini katika mtazamo wa kiroho maisha ni ya kawaida na hayataki mashindano, unashindana na nani? Na unaishi kwa ajili ya nani?  Fanya kile kitu kina manufaa kwako na familia yako ili kesho uje uburudike.  Kwani kuishi ni leo kesho ni matokeo unaweza ufike au usifike, jiwekee akiba kama vile vile unaishi milele halafu muofie Mungu kama vile unaondoka(kufa) leo.

Watu wengi wamechukua muda mrefu kutafuta furaha wameikosa, furaha inaanzia ndani mwako (happiness is inside job) usikae ukisubiri mtu kukupa furaha, utapata ya muda, jiangalie unataka nini na unaweza kufanya nini katika maisha yako?  Jitume sana, fanya sana kazi ili uweze kula matunda mema ya nchi.  Na kumbuka tunaufukuza upepo inabidi tuweze kumshukuru huyu anayetupa pumzi ya bure kwa neema na rehema zake, wengi wanalia, wengi wamekata tamaa, wengi wanataka kujiua na wengine wamesusa hata kuanza tena kwa kuanguka.  Mwenye haki wa Mungu huwa anaanguka mara saba kisha anainuka tena.  
"With God there is second chance"

La hasha wakati ni huu tuamke na tutende yale tuliyoyandika kwenye vitabu vyetu kama ni malengo ya mwaka 2016 najua kuna wengine hawajaandika.  Maandishi yanadumu milele, mazungumzo ni muda mfupi tumia muda wako kuandika malengo yako na uyafanyie kazi.
 "see it, believe on it then you should act on it and you shall see the results as soon as possible"

Hii ni changamoto kwani kila siku angalia umefanya nini na ikifika jioni piga mahesabu ya masaa uliyotumia  kwa kufanya kitu hata kimoja cha maana.

Wako muuinuaji na mtia watu moyo hata kwa yale yanayoonekana magumu, imani pasipo kuona.

Lusako Mwakiluma


Tuesday, February 9, 2016

CHANGAMOTO KWENYE UJASIRIAMALI NA SULUHISHO

Ndugu rafiki, miezi kumi nilipo anza hii biashara nilikumbana na vitu vizito sana katika kuyafikia mafanikio na malengo niliyo lenga ningeyafikia haraka ndani ya biashara ya mtandao!
Nilijaribu kutumia mbinu mbali mbali ambazo kila mfanya biashara wa kawaida hufundisha ktk masomo ya kila siku;
��Niliambiwa ANDIKA MAJINA 100 KISHA TUMA KWA WATU WAKO WOTE UTAPATA MAJIBU MAZURI.
Nilijaribu lakini kilichonipata kiliniidhoofisha zaidi.
��Niliambiwa kila siku nishirikishe watu 5 kwa mwezi nitakuwa na watu 150. Nilijaribu lakini sikupata matokeo mazuri
��Niliambiwa kila siku nitume post moja facebook, nilituma sikuwa napata like hata moja na sikuweza kutengeneza matunda yoyote tofauti na kupoteza muda!


HIZO NI BAADHI YA MBINU NILIZO FUNDISHWA LAKINI SIKUWEZA KUPIGA HATUA KABISA KIBIASHARA. 


Ni dhahiri kuwa wengi tumekuwa tukijiunga na biashara ya mtandao na kuanza,kukimbilia RAFIKI,NDUGU ,JAMAA MBALI MBALI AMBAO TUNA MAZOEA NAO.
��Hilo sio SOKO lililokusudiwa kukupa uhuru wa kipato, ni soko ambalo SIO LA KUDUMU MAISHANI MWAKO!
KATIKA MADA ZETU TUTAKAZO JIFUNZA NI PAMOJA NA KUJUA NAMNA YA KUTENGENEZA KIPATO KISICHO KUWA NA KIKOMO KUTOKA KWENYE SOKO LILILOSAULIKA.
Kuna njia kuu mbili za kutengeneza pesa ndani ya biashara ya mtandao baada tu ya kujiunga
1. Watu ambao tayari wameshajiunga na biashara hii ya mtandao, ndani ya kampuni yako au kampuni nyingine.
Kuna njia ambazo ni rahisi ambazo zitakusaidia kupunguza gharama na kukupa faida kubwa ambayo usingetegemea kuipata!
2. Watu ambao WANATAFUTA FURSA YA BIASHARA YA MTANDAO.
Ni watu wengi wanatafuta fursa hii kila kukicha, hivyo ni jukumu lako mkufunzi kumwonesha mteja wako kuwa unaweza kumfikisha katika ndoto.
Unajua mteja HUCHAGUA MTU GANI?
~Huchagua kiongozi ambaye atamfikisha kwenye ndoto zake na kuishi maisha ya ndoto zake
~Huchagua mtu mwenye UTAJIRI WA MIFUMO HALALI YA KIBIASHARA AMBAZO ZINAKATA GHARAMA NA KUONGEZA FAIDA!
Sio hivyo tu unaweza kupanua kipato chako rafiki, KUMBUKA UNAPOJIUNGA UTAKUTANA NA ASILIMIA 98 YA SOKO LAKO (MARAFIKI ULIOTARAJIA KUWASHIRIKISHA) TAYARI WANA BIASHARA ZAO.
Tuta kufundisha namna ya kutengeneza kipato chako kwa kutatua changamoto za WAFANYA BIASHARA WENGI KUWA NA KIPATO KINACHOPITILIZA CHOTE KWENYE MATUMIZI NA KUTOKUWA ENDELEVU.
Nina imani utafurahia ukitatua hili na hebu fikilia ni WANGAPI WANALALAMIKA NA HILI KATIKA JAMII YAKO?
WENGI SANA, NDIVYI HIVYO HIVYO UTAKAVYOTENGENEZA KIPATO KIKUBWA KWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATU ZINAZO WAKUMBA KUHUSU ELIMU YA PESA!
Nitafurahi kuungana nami kuweza kutumiza ndoto zako kwa kuungana nami

Monday, February 8, 2016

MAMBO SITA YANAYOWEZA PELEKEA UMASKINI

 
Watu wengi wanakufa masikini na wanashindwa kufikia mafanikio yao bila wao kujua tatizo ni nini,imekuwa kama ugonjwa watu wengi kuendelea kulalamikia serikali au wazazi wao kuwa wao hawafanikiwi wao ndio sababu,na wengine wamekuwa wakikata tamaa kabisa ya mafanikio yao bila wao kujua nini kinachokwamisha maisha yao kuwa bora.Leo tutajifunza pamoja vizuwizi vya mafanikio yako ambapo kama utavifanyia kazi basi utaanza kushuhudia mafanikio yako,ni muujiza mkubwa sana utatokea kwako hakuna aliezaliwa kuwa masikini rafiki.soma kwa makini.

1.UOGA(Fear)
Hichi ni kikwazo kikubwa sana kwa watu wengi ktk mafanikio yao,watu wengi wamekuwa masikin na wengine kufa masikin kwasababu ya uoga,uoga wa kukataliwa na uoga wa kushindwa,kama unataka kufanikiwa ktk kila kitu kwenye maisha yako usiogope kuomba au kusema chochote mbele ya watu eti kwa kuogopa kukataliwa rafiki usiusemee moyo wa mwenzio usiogope,lkn pia usiogope kushindwa yani mtu anataka kufanyabiashara lkn kitu  cha kwanza anawaza ni kushindwa anaamini kuwa yeye hawezi na akianzisha atafeli.Rafiki acha uoga kwani huo ndio umasikin wako ushinde uoga ushinde maishani.USIOGOPE..
2. KUKOSA MSUKUMO (Lack of agressivenes)
Watu wengi wanashindwa kufanikiwa ktk maisha yao kwa sababu ya kukosa msukumo binafsi,ngoja nikwambie rafiki hakuna mtu yeyote ambae atakaa chini na kupanga maisha yako au kuna mtu ataacha shughuli zake kwaajili ya kupigania maisha yako,wewe ndio unaejua ugumu na uchungu wa maisha yako amka sasa kuwa na msukumo kutoka moyoni mwako wa kushinda maishani usisubiri fulani ndo akwambie nenda kazi,fanyabiashara wewe mwenyewe kaa chini jitume utafanikiwa.
3.UJASIRI NA KUJIAMIN (Courage and confidance) 
Hpa ndipo balaa watanzania wengi hawajiamini rafiki hebu jiamini kuwa wewe unaweza ndani yako kuna mtu mkubwa saana,hebu acha kusikiliza watu wengine wanasema nini kuhusu wewe usikilize moyo wako      unasema nini kuhusu wewe,usikubali kushindwa thubutu kwa kila jambo unaloambiwa lenye mafanikio na usiamini kuwa wewe huwezi unaweza rafiki.
4.KUKOSA LENGO MAALUMU (Lack of purpose driven goals)
Rafiki malengo yako nini? Lengo ni ndoto zenye mipaka,kuna malengo ya muda mfupi,muda mrefu na muda wa kati.wewe malengo yako ni yapi? rafiki hautakuja kufanikiwa ktk maisha yako kama huna malengo ya maisha yako kama huna malengo panga leo yaandike malengo yako.mtu asiye na malengo ni sawa na mtu ambae anaenda stendi kupanda gari lkn hajui anaenda wapi sasa atapanda gari gani na atashukia wapi huyu hata fika bali atazunguuka a ari hadi usiku gari linapokwenda kupaki basi litamshusha popote.JUA MALENGO YAKO RAFIKI UTAFANIKIWA.
5.KUTOKUJITOA (Lak of comittment)
Kujitoa limekuwa tatizo kwa watanzania wengi, ewe mtanzania jitoe kwaajili ya maisha yako acha uvivu wa kufikiria Mungu ashughuliki na wavivu jitoe pambana kwaajili ya maisha yako utafanikiwa. 
6.KULINDA MUDA (Timemanagement)
Hahahahaaaa watu wengi wanaposikia mua ni mali huwa hawaamini leo nataka ujue kuwa muda wako ndio umasikini wako na ndio utajiri wako.unatumiaje muda wako ambao unatoka kazini? unatumiaje muda wako ambao unatocha chuo? wewe mama wa nyumbani unatumiaje muda wako ambao unakuwa hauna kazi nyumbani? hapa ndipo kasheshe na umasikini wa watu ulipo.iko kila sekunde na saa inayopita lazima uhakikishe unafanya kitu ambacho chenye manufaa kwenye maisha yako,mfano ukitumia masaa mawili unajifunza kitu chenye mafanikio kwenye maisha yako basi unayavuta mafanikio yako masaa mawili kama mafanikio yako yalikuwa uyafikie kwa siku mbili na masaa mawili basi utakuwa umebakisha siku mbili.kama unatumia muda wako kuangalia TV,kupiga umbea kupiga story zisizokuwa na maana ukifanya hivyo masaa mawili kwa siku ndani ya mwaka utakuwa umepoteza zaidi ya miezi 4,basi hiyo miezi minne ndio umesogeza mbele mafanikio yako.kwaiyo kama ungetakiwa ufanikiwe kwa miaka miwili basi utafanikiwa kwa miaka miwili na miezi minne.sasa watanzania wengi huwa wanapoteza zaidi ya miezi 9 kila mwaka ndani ya miaka 15 tayari ameshasogeza mbele mafanikio yao kwa zaidi ya miaka kumi.kwa hiyo ukichukuwa miaka kumi ya kutafuta maisha na ile miaka kumi aliopoteza ni miaka 20.ameanzakutafuta maisha na miaka 30-40 miaka ya kufikia mafanikio yake itakua 50 na maisha now ni mafupi hayafiki huko na kipindi anaendelea kutafuta anapoteza tena masaa kadhaa.lazima ufe masikini.amka sasa mtanzania acha kutumia muda wako vibaya kwani muda wako unaoupoteza sasa utakugharimu.
MUDA NI MALI UKIPUUZA HILO UTAKUFA MASIKINI.ACHA KULALAMIKA CHUKUA HATUA.
Karibu tutimize ndoto zetu pamoja.
SOURCE:BASSANGA CHANGING LIFE
 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7