BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Tuesday, December 27, 2016

WEZESHA TRUST FUND - MOROGORO YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA

WEZESHA TRUST FUND WALIPOTEMBELEA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA BIGWA - MGOLOLE
TAREHE 26/12/2016. 
WALITOA MISAADA  MBALIMBALI KUSHEREHEKEA SIKU YA KUFUNGUA ZAWADI 
 PAMOJA NA WATOTO HAO   
WALITOA MISAADA YA SAMAKI, NYAMA, MATUNDA, SABUNI, SUKARI NA VINYWAJI MBALIMBALI  


Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund - Morogoro wakisaini kitabu cha Wageni Bigwa Mgolole - Kituo cha kulelea watoto yatima kutoka kushoto Mkurugenzi Bi Lusako Mwakiluma, Daktari Dr Elias Yuda Mtungilwa, Msaidizi wa Utawala na Mwalimu wa Tehama Maines Richard, Afisa Mafunzo Mohamed Nyongo.

Wezesha Trust Fund wakifurahi pamoja na  Sista mlezi pamojawatoto yatima mara baada ya kukabidhi misaada, watoto walifurahi sana kupokea zawadi zao.

Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund wakiwabembeleza watoto yatima ambao ni wachanga wanaolelewa katika kituo hicho, 

 Wezesha Trust Fund kwa pamoja inaiomba jamii kuwa na tabia ya kuangalia watoto kama hawa katika vituo vilivyo karibu na mbali kwani ni faraja kubwa kuhakikisha yatima wanapata furaha kama watoto wengine.  Yatima ni watoto wetu tusiwatenge wala kuwabagua.
Wezesha Trust Fund wakiwa pamoja na watoto yatima wa darasa la kwanza na pili - kituoni hapo wakiongozwa na Derick na David(mapacha) ambao tangu wakiwa na siku tatu baada ya kuzaliwa na kufiwa na mama yao Wezesha inawatembelea na kila wanapowaona wafanyakazi wa Wezesha wanafurahi sana.
Mungu wabariki walezi wa watoto hawa yaani Masista wote wanaohusika na pia wabariki watoto yatima wote wakue katika maadili mema na kumtegemea Mungu.

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7