BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Friday, January 20, 2017

WEZESHA TRUST FUND WALIPOFANYA ZIARA KWA WAHANGA WA MAFURIKO WILAYA YA KILOSA MEI, 2016

Wafanyakazi wa Wezesha Trust Morogoro walipotembelea Wilayani Kilosa kuwapa pole wahanga wa mafuriko Wilayani Kilosa.  Mafuriko hayo yalitokea mwanzoni mwa mwaka 2016.  Wezesha ilitoa pole kwa misaada ya nguo, chakula na pesa taslimu.  Pia Wezesha walienda kuangalia eneo lililoathirika na mafuriko kijijin na mto wa Tindiga ambao ni  chanzo cha mafuriko.
                               
Mkurugenzi wa Wezesha Trust Fund Bi Lusako Mwakiluma akikabidhi misaada kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mheshimiwa Henjewele Mei, 2016, misaada iliyokabidhiwa ni chakula, nguo, fedha taslimu na vitu mbalimbali.
Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya Henjewele akishukuru Asasi ya Wezesha na wadau wote waliochangia hali na mali kuhakikisha misaada inapatikana na kupelekwa Kilosa kwa wahathirika wa mafuriko.  Mungu awabariki wote waliotoa kwa upendo misaada hiyo.

Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa wakishusha misaada toka kwenye gari baada ya Wezesha kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kilosa.  Aliyekuwa Katibu Tawala wa Wilaya aliongoza ushushaji wa misaada hiyo.
Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund walipokuwa Kilosa mara baada ya kukabidhi misaada hiyo kwa Mkuu wa Wilaya kutoka kushoto Mohamed Nyongo(Kaimu Afisa Mafunzo), Janeth Lupupa(Afisa Mafunzo) na Abuubakari Mkingiye(Mratibu wa mambo ya nje) wanaiomba jamii kujitoa kwa hali na mali katika matukio yoyote yanayowahusu watu wengine kwani wanaamini kutoa ni moyo wala sio utajiri.

Wafanyakazi wa Wezesha wakitathmini athari za mafuriko katika nyumba za wenyeji ambao walizikimbia baada ya mafuriko kutokea kutoka kulia ni Mohamed Nyongo(Kaimu Afisa Mafunzo) na Salum Tindwa(Mratibu wa Miradi) Wezesha Trust Fund.  Kwa kweli hali ilikuwa ni mbaya lakini Mungu amesaidia wahathirika wako sehemu sahihi kwa muda huu.

Nyumba iliyoathirika na mafuriko ikiwa imeezuliwa paa na uharibifu mkubwa, maji yaliingia ndani ya nyumba kiasi cha 3/4.

 Watoto walioathirika na mafuriko wakiwa wanacheza eneo la tukio kwani imekuwa kama jangwa, mazao yalipotea, mkondo wa maji umeharibu shule, makanisa na hata sehemu za watoto kucheza.
 Wamama waliothirika na mafuriko wakiwa wanatoka kuchota maji mbali na makazi yao, kisima cha maji kilizibwa na matope makali  na ikafikia mahali maji yalikuwa shida, lakini Mungu ni mwema wameviona baadhi ya visima na wanaendelea na maisha mahali hapo.

Wezesha Trust Fund inawaomba watanzania, wanajamii  na wadau wote kwa ujumla kujitoa kwa uadilifu katika kila janga linalowapata wenzetu.  Jamii yetu ni wamoja tupendane na kutendeana yaliyo mema na Mungu wa Mbinguni atatulipa.

Lusako Mwakiluma
Mkurugenzi 



Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7