BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Sunday, January 1, 2017

SABABU ZINAZOPELEKEA WANAWAKE KUWATEGEMEA WANAUME JAPOKUWA WANA FURSA NYINGI SANA

Fursa za wanawake  ziko nyingi sana lakini wanawake wenyewe hawana motisha ya kuzikimbilia na kwenye uzalishaji mali wako vizuri sana ila tu kuna baadhi ya wanawake ni waoga kujaribu nab ado wanaamini kuwa mwanaume ni mtafutaji na mwanamke ni mama wa nyumbani siku zote.  Hii inaonyesha mwanamke akiishi bila mume  au akikimbiwa na mwanaume anashindwa kusimama kwa hofu  ya kushindwa maisha.  Kuna fursa za kibiashara, ufugaji na utengenezaji bidhaa mbalimbali ambazo kila siku zinajitokeza lakini katika suala la kujifunza wanawake ni wazito na hata kuuliza kama kitu hawawezi pia ni taabu.

Wezesha Trust Fund inatumia njia nyingi katika kuwaelimisha wanawake:  Inatumia Television, Redio, semina na warsha za mara kwa mara. Wanawake wengi  wanatambua kuwa kila mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake yuko mwanamke na ukikuta mwanamke kafanikiwa ujue nyuma yake yuko peke yake.  Wanawake pia wana majukumu mengi ya kifamilia na ya kibiashara, apike, afue, aende kazini, anyonyeshe na pia amhudumie mume na watoto.  Muda wake ni ule ule na kazi ni nyingi, kuna muda anachoka kwani naye ni binadamu.

Wakati naongea na wanawake hawa nakutana na changamoto nyingi wanazopitia wanalalamika wenyewe kwamba hawajiamini, waoga, na wakiona biashara kidogo zinasumbua wanaacha.  Na kuna wengine mitaji inakata kwa sababu ya waume zao wanawaachia majukumu ya nyumbani na pia wanaume hao hao hawawapi fursa wanawake zao za kufanya biashara kwa upana zaidi. Pia wengine wanawakataza wasitoke majumbani kwenda kwenye biashara.  Wapo wanawake wengine wao makundi yanawaharibu wanaishi maisha ya kuiga na kutamani vitu nje ya uwezo wao.

Ushauri wangu adui wa mwanamke ni yeye mwenyewe na pia kutokana na mfumo  uliopo tangu awali  wanawake ni viumbe hafifu na wengi wanafahamu hivyo na hawataki kuchukua hatua, wainuke na waseme hapana inapobidi kusema hapana. Wanaume nao nawaomba waache kuwakatisha tamaa wake zao  bali wawatie moyo kwani wanawake wakitiwa moyo na nguvu wana ujasiri kuliko hata wanaume, pia kuna wakati wawasaidie majukumu ya nyumbani kama yanakuwa mengi.  Pia wanawake ni wazuri katika kutunza fedha.  Nawaomba wanawake wenzangu wajidhatiti katika kusimamia kile walichonacho ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea ya maendeleo.  

Wezesha na wadau wengine hatutaacha kuwatia moyo wakati wote watakapohitaji ushauri wa kitaalamu. Kauli Mbiu yetu siku zote: “Wakiwezeshwa wanaweza

Karibuni tulishirikiane kulijenga Taifa letu kwa bidii na maarifa.

Lusako Mwakiluma

Mhamasishaji na muinuaji waliokata tamaa

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7