BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Sunday, March 20, 2016

FIKIRIA KAMA MBUNIFU ILI UWE MTU MWENYE UMAKINI WAKATI WOTE

Wakati unafikiria mawazo yako ya ndani ni kwamba uko tayari kuzalisha kitu kizuri ulichobuni kama mbunifu;  Wakati wote unatakiwa kuwa hivyo ili uweze kuleta kitu cha tofauti katika jamii. Waangalie wabunifu wakubwa walioweza kutumia umakini na kuweza kubuni baadhi ya vitu ambavyo leo tunavitumia;-

Thomas Edison alifikiria akapata wazo kubadilisha ulimwengu wa Technolojia
Albert Eistein alifikiria akapata wazo la kubadilisha ulimwengu wa fizikia
Charles Darwin alifikiria akapata wazo la kubadilisha ulimwengu wa biolojia

Sio wote kwa upande wetu wanafanikiwa kwa kiasi cha kupata wazo zuri, tunaangalia kwa kufikiria ubunifu, mawazo mazuri na kupata suluhisho la jambo.

Kufika hapo unatakiwa uende kufikiria kila siku na uangalie ubunifu wako wa ndani kwa kutengeneza mawazo mengi na kuchukua kama tahadhari kama inawezekana.

Hapa angalia jinsi ya kutengeneza mawazo kama mbunifu:
Fikiria sana
Tengeneza mawazo mengi, mbadala na mwisho wake kama inawezekana usiwe na wasiwasi kuhusu  ubora wa wazo lako, ila ni mawazo mangapi unaweza kuwa nayo.  Kuna muda wa kuangalia tena baadaye na hata kama umemaliza kuyaangalia mawazo yote.  Kitu unachokitaka hapo ni kupata wazo moja tu kubwa.
Usijihukumu
Hata kama ukoje au upendi mawazo yako yaache yaje.  Kuangalia somo la nyuma kwa macho mapya, kama ulipitia kwenye hali hali ngumu jaribu kutazama kwa mtazamo mwingine mpaka upate wazo moja zuri. Hii itakusaidia kufikiria kitu katika ufahamu wako ambao huru, usijihukumu.
Tengeneza orodha
Andika chini au pengine tunza kwenye kumbukumbu kila wazo, hata kama unaona sio wazo zuri kwako.  Tena  wazo baya  unaliweka pamoja kwani ndani yako sio yote mawazo mazuri kama linakuja liweke tu unaweza ukalitumia mahala fulani na usijiweke katika sehemu ya kuchanganyikiwa kuhusu mawazo yako, subiri au  jiulize ni wazo langu mwenyewe? Baadaye unaweza ukaitumia hiyo orodha kupata faida kubwa.

 Changanua mawazo yako na uyaboreshe
Njoo na mtazamo wa wazo lako kwa kulipanga bila kufuatana au kutokuwa na umuhimu.  Angalia njia mbadala ya kufikiria kuhusu  somo hata kama  ni njia ya zamani lakini inafanya kazi.
Pika wazo lako na  na liiache liendelee mpaka lizalishe kitu
Panga muda  wa kupika  mawazo yako na yaruhusu  yaweze kuendelea kuzalisha mawazo mengine hii inachukua muda.  Fanyia kazi tatizo, tengeneza wazo, tena tembea  na fanya kitu kingine kabisa tofauti. Usifikirie kuhusu tatizo  wakati mwingine ila liache nyuma tatizo likiungua polepole. Unaweza ukashangaa ni wakati gani ndani kitu kinafanyika chenyewe, wakati wewe umeacha kiendelee chenyewe.

Wote tunataka kupata ubora mzuri na mawazo mazuri katika kila tunachokifanya.  Ili kuboresha njia nzuri ni kufikiria sana na jinsi tunavyojiongoza na jinsi tunavyoutunza muda wetu, hatua ya kwanza ni kuboresha  tunavyofikiria.  Je, unafahamu hivyo? Nakwambia utakuwa mtu mwenye umakini katika kila unachokifanya wakati mwingine popote ulipo.


Lusako Mwakiluma

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7