BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Sunday, December 25, 2016

JE, KUWA TAJIRI KUTAKULETEA FURAHA

Kwa nini unataka kuwa na pesa nyingi, je pesa nyingi zitakupatia amani au furaha? 
Kuwa na pesa nyingi itakupatia amani.   Kama utakuwa na pesa nyingi  utalipa madeni yako yote, utakwenda popote unapotaka kwenda na utafanya chochote unachotaka kufanya.

Ninachotaka kukufahamisha  hapa ni kwamba kuwa na pesa nyingi itakusaidia  kuponya vitu vyote?  Usije ukaanguka mwenyewe kwenye eneo la kufikiria. Kama unafikiria pesa itakupatia furaha, utakuwa unajidanganya mwenyewe.

Hauwezi kuwa na furaha utakapokuwa na pesa nyingi labda unaweza kuwa na furaha usipokuwa na pesa.  Kama ni mtu mwenye kumaanisha, kuwa tajiri kutakufanya uwe na uhuru wa kujiamulia mambo yako mwenyewe kwa kile ulichonacho kwa wakati ule.  Kama utakuwa mtu mwenye huzuni, kuwa tajiri utakuwa  umejipa uhuru wa kuitafuta furaha yako kwa wakati huo.

Kuwa tajiri ni kwamba tayari umeshaandaa kiasi cha pesa ambacho ulikitafuta.  Ufahamu wako utakuwa unajihakikishia kuwa mtu ambaye hapo mwanzo haukuwa hivyo na cha muhimu ni kuvunja sheria ya kujipangia matumizi yako ya pesa kabla ya kuishika mkononi.
Mfano:   30% kwa ajili ya matumizi ya kuishi
                30% kwa ajili ya matumizi ya kuweka akiba
                30% kwa ajili ya matumizi ya starehe na furaha ya  familia
                10% kwa ajili ya kuwapatia wasionacho
Asilimia mia moja (100%) ya kila pesa yako igawanye katika mafungu manne.

Kitu cha muhimu sana ni kufanya kazi kwa bidii yako mwenyewe kuliko kufanya kazi kwa ajili ya kutafuta utajiri.  Ni muhimu kufanya hivyo kwasababu kiasi cha utajiri  wa mtu alichonacho hakiwezi kuzidi  maendeleo yake binafsi.
Ngoja nikupe mfano:  Ni mara ngapi unasikia mtu ameshinda bahati nasibu na amepata kiasi kikubwa cha pesa?  Halafu baada ya muda mfupi unasikia zile pesa zote zimeisha kwa muda mfupi sana.

Kumbuka alikuwa anasema kabla ya kuzipata pesa hizo.  Kama nikishinda kiasi kikubwa cha pesa kwenye bahati nasibu nitafanya kitu kikubwa na nitakuwa tajiri mkubwa sana, kumbuka alisema wakati hajazishika hata wewe wakati hauko na pesa unasema nikizipata.  Je, umepanga chochote kabla ya hizo pesa kupatikana au utapanga ukishazipata? Utafiti unaonyesha kwamba bahati nasibu ni kitu kinachojulikana sana na watu wanaamini katika bahati nasibu kwa sababu mbili:
            1. Mpango wa pesa za haraka haraka
            2. Pia ni mchezo wa furaha

Ni mchezo unaochezwa kila siku leo unaweka pesa kidogo na kesho unapata kiasi kikubwa basi ni kitu endelevu na watu wanategemea kuna siku nitapata zaidi ya jana.  Hii inakuhakikishia kama utapata basi utamaliza shida zako zote. Na yale yaliyosimama yote yatafanikiwa kwa urahisi. Watu wengi wanaandaa kesho yao kwa kujinyima leo ili kesho yao iwe nzuri zaidi.

Hauwezi kuwa tajiri mpaka uvunje sheria kwa kujihakikishia kila pesa yako unayoipata unaivunja mara nne ili uweze kutimiza azma yako uliyojiwekea. Nitakuletea mpango mzima wa kuwa tajiri kwa haraka kwa kuvunja sheria.

Karibu sana tuchangie hoja, tutoe maoni na tujihakikishie kufika pale tunapopataka.

Lusako Mwakiluma
Mhamasishaji na Muinuaji kwa waliokata tama
Wezesha Trust Fund - Morogoro

26 Desemba, 2016


Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7