BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Sunday, December 11, 2016

NJIA TANO ZA KUONGEZA UJASIRI WAKO

1.   Chagua watu wenye ujasiri na wenye hari ya chanya ndani yake
Kaa na watu wenye ujasiri, ukikaa na watu wenye ujasiri nawe utakuwa jasiri kwani utajifunza kupitia wao kumbuka hata Biblia inasema enenda na wenye hakima nawe utakuwa na hekima mithali 13:20 lakini rafiki wa wapumbavu atahangamia.

2.     Fanya kila siku kitu kinachokufurahisha au kukifurahia. 
Ukifanya kitu ambacho haupendi kufanya hauwezi kutunza ujasiri wako, utakuwa unafanya huku haujiamini.  Fanya kile kitu roho yako inataka na utaona unakifanya katika hari kuu na kubwa sana.

3.     Zingatia malengo na mipango uliyojiwekea
Malengo ni muhimu sana katika maisha ya kila binadamu.  Kama hauna malengo basi amini kwamba ufahamu wako umekufa.  Malengo na mipango yako ndiyo inayokupelekea kufika mbali kimaisha.  Hauwezi kufanya mambo kiholelaholela.  Mipango ndiyo matumizi yako ya kila siku.  Mipango na malengo ni dira ya mafanikio yako.  Andika kwenye daftari au kitabu malengo yako kisha uyafanye kwa mpangilio unaoutaka kwa muda uliojiwekea.

4.     Usikate tamaa
Katika safari ya maisha hakuna kukata tamaa na mtu jasiri hakubali kushindwa kwa lolote.  Hivyo hata kama unaona kuna kushindwa usikate tama kabisa.  Songa mbele uweze kuiona siku nyingine na mwisho kufikia malengo uliyojiwekea.

5.     Tumia muda wako vizuri
Muda ni pesa, na wakati ni mali masaa 24 tuliyopewa na mwenyezi Mungu wote tunayo.  Iweje tajiri afanikiwe kwa masaa haya haya 24 na wewe ushindwe katika masaa haya 24 inabidi ujiangalie tena na tena.  Pia usiogope kujaribu kwa kuhofia kushindwa kwa muda uliopo, unaweza ukashindwa kumbe ndiyo ushindi wako unapoanzia. 

Karibu sana tuendelee kuinuana na kutiana nguvu.

Lusako Mwakiluma
            (Motivational & Inspirational speaker)
                 


BOFYA KUPATA HABARI YA KUMJALI MTEJA

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7