BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Sunday, December 11, 2016

FORTUNE TEAM WAKIFANYA USAFI SABASABA HOSPITAL - MOROGORO


Wezesha Trust Fund wakiwafundisha kazi za kujitolea Fortune Team kutoka shule ya sekondari Uwanja wa Taifa siku ya 1 Desemba, 2016 kuazimisha siku ya Ukimwi Duniani, Timu ya Fortune inafahamu jinsi ya kusema hapana na kujikinga na VVU/Ukimwi wakiamini Vijana bila ukimwi inawezekana.

Fortune Team wakiendelea na kufanya usafi kwa kujitolea kama walivyofundishwa na Wafanyakazi wa Wezesha Trust Fund - Morogoro
Fortune Team wakiendelea na usafi baada ya kuhitimisha mafunzo yao ya siku Moja ya kuepuka na kujikinga na Ukimwi mashuleni.

Mkurugenzi wa Wezesha akihakikisha kwamba usafi unafanyika kwa kiwango cha hali ya juu katika Hospitali ya Sabasaba ndani ya kata ya Uwanja wa Ndege.


 Mohamedi Nyongo afisa  Mafunzo akishirikiana na Fortune Team kufanya usafi kwani mtoto umleavyo ndivyo akuavyo na mifano ni lazima kwa wanafortune team.  Mungu ibariki Wezesha na Mungu ibariki Fortune Team.
 Mkurugenzi wa Wezesha Trust Fund akihojiwa na Vyombo vya habari kuhusiana na siku hiyo.  East Africa Radio na Television walikuwepo pia SUA Television walisimama kidete kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa sawa.
Afisa Tawala Bi Mainess Derick akiwa pamoja na Fortune Team kwa msisitizo wa siku ya Ukimwi Duniani wakiamini kuwa maombukizi mapya ya Ukimwi kutoongezeka na kuhakikisha yanapungua kama sio kumalizika.

Ilikuwa ni siku ya Ukimwi Duniani 1 Desemba, 2016

Fortune Team ni wanafunzi toka Shule ya Sekondari Uwanja wa Taifa waliojiunga na Wezesha Trust Fund kama mabalozi wa wanafunzi wengine katika kuhakikisha wanafuata maadili ambayo nao wamefundishwa na kuelimishwa na Wezesha Trust Fund - Morogoro ikiwa ni muendelezo wa kazi ya kuwaelimisha Vijana rika kuweza kufanikiwa katika malengo yao waliyojiwekea kwa kuepuka vishawishi toka kwa wanawake na wanaume, mimba na ndoa za utotoni, Semina ilifanyika tarehe 19/11/2016 katika Ukumbi wa Pastor Phil Training Centre.

Mambo matano waliyojifunza:

1. Elimu ya Kujitambua
2. Jinsi ya kuepuka mimba na ndoa za utotoni
3. Elimu ya Ukimwi na VVU na jinsi ya kuepuka
4. Jinsi ya kusoma na kufaulu kwa kiwango cha juu
5. Elimu ya kufanya kazi za kujitolea

Wezesha pia inawashukuru Viongozi wa Mkoa wa Morogoro kwa ushirikiano wa siku hii ya usafi kwani ilikuwa ni kuwafundisha vijana hawa kufanya kazi ya kujitolea katika jamii kwa hiari yao.  Tunashukuru Mkurugenzi wa Manispaa, Mganga Mkuu wa Mkoa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sabasaba kwa ushirikiano waliotupatia.  Tunasema asante sana.  Kauli mbiu ya siku ya tarehe 1 Desemba, 2016 saidia kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi. 

BOFYA HAPA KUONA TUKIO LA SIKU YA WEZESHA

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7