BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Tuesday, February 2, 2016

ZIELEWE CHANGAMOTO ZA MAISHA

 Kwa sababu tumeumbwa tofauti, wako walioumbwa kushughulika na mambo ya wenzao tu muda wote wanaangalia fulani kafanya nini na kafanikiwa au kashindwa kwa kiasi gani.  Mwisho wa siku ukiwaangalia watu hawa utajikuta unashindwa kufikia malengo yako na kukwama njiani katika safari yako ya maisha.  Ndugu yangu simama katika nafasi yako na usiwaangalie walioshindwa, walioshindwa wana maneno mengi sana.  Na ukiwafuata watakupotezea dira kabisa.  Amini kile unachokifanya na amini kwamba kitafanikiwa kwa asilimia mia moja pamoja na hali zilizopo usirudi nyuma Mungu ni mwema kwetu siku zote na yeye anaangalia mwisho wako sio mwanzo wako. 
 Kuna watu wameumizwa, kuna watu wameachwa, kuna watu wamekimbiwa na kuna watu wamefiwa na kukataliwa na kuonekana si kitu kwenye jamii zao zinazowazunguka.  Nakuomba ndugu yangu usifikirie kujiua au kususa kwa ajili ya maisha yako simama ukijipa moyo kwamba wewe sio wa kwanza unayepitia haya mama yangu nimpendaye sana Maya Angelou mwandishi wa vitabu na misemo yake mizuri alisema katika mahojiano yake na Oprah Winfrey “kwamba kila unachopitia amini sio wa kwanza kukipitia wapo waliopitia unayopitia tafuta njia mbadala na kisha endelea mbele” nakwambia muda sio wetu hata kwa kuuza maji ya mia mia utatoka tu.  Usikae chini na kukata tamaa utapoteza dira yako.
Hayo yaliyopita chukulia kama changamoto na hao waliokuacha na kukumbia wachukulie kama ngazi ya kupandia kuelekea kwenye mafanikio yako na yachukulie ya jana kama historia ya kuja kuwashuhudia watu waliokuwa na hali kama hizo kwa baadae.  Amina tu na songa mbele kwani adui ni ngazi ya kupandia na unaombwa kila siku kumpenda adui yako, jiulize je., huyu adui yangu akifa huyu nani atakuja kunipigia makofi wakati naenda kufanikiwa na kuwashuhudia wengine nilikotoka?.  Kuwa na roho ya unyenyekevu na ya msamaha kwa yeyote anayekwenda kinyume na wewe kwani hakuna barabara ndefu bila kona na hakuna yaliyo marefu bila kuwa na ncha.  Kumbuka kwa wale wakristo Danieli, Meshack na Abelnego waliwekwa kwenye tanuru na hawakuungua kwa sababu ya imani ya Mungu wao waliyemwamwini kwanini usiwe wewe ule moto ni changamoto kama hizi ninazokuhadithia hapa.  Naamini kuna watu wanaenda kupokea miujiza yao ya mafanikio kupitia changamoto hizi za maisha nasema maisha ni rahisi kama unayapatia na ni magumu kama unapoteza muda kuangalia tatizo badala la suluhisho la tatizo lako.  Jiulize Bill Gates, Obama, Hillary Clinton wao wamezaliwa na nani na wananguvu gani za kukushinda wewe ambaye una masaa hayo hayo na nguvu kama zao.  Inuka twende mbele tusipoteze muda wala saa.
Nakutakia usomaji mwema wa mada zangu na Mungu atakuinua kwa namna ya tofauti mpendwa. 
Karibu sana
Lusako Mwakiluma

Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7