BREAKING NEWS

VIDEO

BIASHARA

USHAURI WETU

Monday, February 29, 2016

MAISHA NI RAHISI SANA UKITULIA NA KUTAFAKARI

Napenda kutoa mada fupi na ya kutiana moyo wenyewe kwa wenyewe, kwa mtazamo wa macho ya nyama maisha ni magumu sana, lakini katika mtazamo wa kiroho maisha ni ya kawaida na hayataki mashindano, unashindana na nani? Na unaishi kwa ajili ya nani?  Fanya kile kitu kina manufaa kwako na familia yako ili kesho uje uburudike.  Kwani kuishi ni leo kesho ni matokeo unaweza ufike au usifike, jiwekee akiba kama vile vile unaishi milele halafu muofie Mungu kama vile unaondoka(kufa) leo.

Watu wengi wamechukua muda mrefu kutafuta furaha wameikosa, furaha inaanzia ndani mwako (happiness is inside job) usikae ukisubiri mtu kukupa furaha, utapata ya muda, jiangalie unataka nini na unaweza kufanya nini katika maisha yako?  Jitume sana, fanya sana kazi ili uweze kula matunda mema ya nchi.  Na kumbuka tunaufukuza upepo inabidi tuweze kumshukuru huyu anayetupa pumzi ya bure kwa neema na rehema zake, wengi wanalia, wengi wamekata tamaa, wengi wanataka kujiua na wengine wamesusa hata kuanza tena kwa kuanguka.  Mwenye haki wa Mungu huwa anaanguka mara saba kisha anainuka tena.  
"With God there is second chance"

La hasha wakati ni huu tuamke na tutende yale tuliyoyandika kwenye vitabu vyetu kama ni malengo ya mwaka 2016 najua kuna wengine hawajaandika.  Maandishi yanadumu milele, mazungumzo ni muda mfupi tumia muda wako kuandika malengo yako na uyafanyie kazi.
 "see it, believe on it then you should act on it and you shall see the results as soon as possible"

Hii ni changamoto kwani kila siku angalia umefanya nini na ikifika jioni piga mahesabu ya masaa uliyotumia  kwa kufanya kitu hata kimoja cha maana.

Wako muuinuaji na mtia watu moyo hata kwa yale yanayoonekana magumu, imani pasipo kuona.

Lusako Mwakiluma


Post a Comment

 
Copyright © 2013 WEZESHA TRUST FUND
Powered by WordPress24x7